MAJALIWA: RAIS SAMIA AMEDHAMIRIA KUIFUNGUA TANZANIA.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuendelea kuifungua Tanzania kwa kujenga barabara katika maeneo mbalimbali nchini ili Watanzania wazitumie katika kufanya shughuli kijamii zikiwemo biashara. Aliyasema hayo jana (Jumatatu, Januari 24, 2022) alipozungumza na wananchi wa Dareda akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali mkoani Manyara.